Friday, 22 April 2011

HOTUBA YA KATIBU MKUU KWENYE KIKAO CHA TAREHE 03/04/2011

Ndugu waalikwa,
Ninayo furaha kubwa ya kua mbele yenu siku ya leo.  Nimelazimika kuchukua mzigo huu mkubwa kabisa wa kuongoza  Emo ‘ya M’mbondo hapa Perth . Kama mwana member wa Emo ni haki yangu ya msingi  kuchagua au kuchaguliwa. Hivo basi, nazani kwa ushurikiano wenu, wote tutaweza kufanya Emo ‘Ya M’mbo Perth kuwa Jamii moja, imara na yenye maendeleo .
Hii ni zamiri yangu tu. Ila watakao lifanikisha hili ni nyinyi. Tunaweza kufikia hapo kwa kubadili tabia  zetu ambazo mizizi yake imejikita kwenye mambo madogo madogo kama vile: misiba, kujifungua kina mama wajawazito, harusi ao tafrija.Hapa namaanisha “ malanda o bonga male malya”.
Kwa sasa lengo la uongozi wetu ni mshikamano ,mipango na maendeleo.  Tujiulize Emo ‘ya M’mondo ilianza lini duniani?  Nani alianza Emo ‘Ya M’mbondo duniani? Iko wapi? Emo iliisha fanya nini kwa Wabembe Duniani ,Australia ,Perth, Congo, au Fizi?
Jibu ya maswali yote hayo ni kwamba, Emo ‘Ya M’mbondo ina historia kubwa. Ilianza tangu kuzaliwa koo za  M’bembe wa Kwanza na  kililenga maendeleo yao. Ila ,hadi sasa maendeleo   wabembe  ni machahche sana duniani ukilinganisha na makabila mengine ambayo ni jirani zetu.
Utofauti wetu ni upi? Ukweli ni kwamba  Wabembe tumeshindwa kupanga miradi ya maendeleo. Ama tukipanga , hatuendelei. Tunayo mifano mingi sana: SOCODEFI, ACCOREFI, ASMAKU, BDC/Mshimbakye, bila kusaau kanisa la Methodist Libre. Ukweli ni kwamba mipango bila mshikamano hakuna maendeleo. Je , leo tunaitaji kupanga kama wale waliotutangulia? Wapi walipo kosea ili tusikosee na sisi ?  Ukweli ni kwamba “kushindwa kupanga ni kupanga kushindwa” ,kama tunavyo sema kwenye Kibembe kwamba “Mbama ya lúkendo ekyo lala ya lúngwa”. Leo natamani kuwaambia mipango yetu.
1.       Mwaka huu kutakuepo na  vikao vya baraza kuu vitatu (Mwezi huu, mwezi wa sita au juna   pia mwezi wa saba). Lengo  nikuchukua maamuzi muimu ya Emo.
2.       Pia tutakua na ziara mbalimbali kwenye ma offisi ili tupate fursa ya kukitangaza Emo kwa wafazili, waisani na wawekezaji  mbali mbali.
3.       Tutakua na seminar mwezi wa  saba . Lengo la seminar hii nikufaamishana mila na desturi za kibembe, maendeleo ya kibembe  na wabembe sehemu mbali mbali . Tutapata fursa ya kuwaita  wabembe wa maeneo mbalimbali ili waje  tubadilishane uzowefu na kujua kile ambacho tunatakiwa kufanya katika ulimwengu huu wa utanda wazi ambao kizazi cha kwanza cha M’mbondo akikupata bahati yakuona.
4.       Tutakua pia na sherehe za kumbukumbu ya  Mauwaji  ya makobola ilio fanyika tarehe 29 -31 /Dec.1998. Hii fursa tutaitumia kufaamisha ulimwengu mzima kilichotufanya tuache maskani yetu nakuweza kujikuta hapa Australia.
5.        Hatutaishia hapo tu, tuna lengo la kukusanya Dollar 10,000 (elfu kumi) mwaka huu  ili tuweze kuwa na miradi mbali mbali ya maendeleo kama vile Shop na Centre Culturel  ya Wabembe.
6.       Tutakua pia na maswala mbalimbali ya Jamii: Kina mama, vijana, wazee. Tutaweza kutembelea kina mama walio jifungua  na watu wenye matatizo mbalimbali.
7.       Uchaguzi wakamati mpya itakuepo mwezi  wa kumi na mbili.
Ndugu zangu,
Kazi hii ni kubwa sana  kama mutaikubali. Inaitaji msaada wenu. Msaada wa hali na mali kufanikisha hili. Naomba kamati kuu irizie mabadiliko yafuatayo kwenye katiba:
1.       Sheria ya mapato na usimamizi wa fedha: Kila mwana member atakaye shindwa kutowa mchango wake wa iyari ,achukuliwe hatua za kinizamu kama kusimamishwa uwana chama wake  na  kunyimwa haki za uwana chama kama  kuchagua na kuchaguliwa .
2.       Sheria ya Matumizi ya Chama: Tunapo jikuta kwenye bank tuko na dollar 3,000 bila kujua tufanye nazo nini ndo hapo tuna nunua kile ambacho hatuitaji. Tunavitu kwenye Emo , ambavyo si vya lazima au havitumiki : Guitars, Keyboard ,etc. Hivi vitu ni lazma tuvifanyie kazi. Ivyo basi, tunaomba Watendaji wa chama wawezeshwe ili kazi yao iwe yenye kukamilika: usafiri na mawasiliano.
3.       Malipo au Michango ifanyike directly kwenye Account ili kupunguza  usumbufu.
4.       Kila mwisho wa mwaka , members  wapewe Certificates of donation ili wapate ku claim donation tax rebate.
5.       Emo iwe na Muhuri wake kama Chama.
Ndugu zangu,
Mambo mengine yanaweza jitokeza  hapo baadaye. Mabadiliko tutakabiliana nayo. Nawakilisha hoja  Kamati  kwenu kama Baraza kuu ili muweze kujadili .Túle bani ,tuikange ifumba.
Asante.
Maitre Philbert Bilombele,  A. (MIR)
Katibu Mtendaji.

1 comment:

  1. Habari zenu
    Mimi mi mbembe nipo Tanzania kwa hakika nimefurahishwa na hatua mnazochukua baada ya kufika huko nchi za watu

    ReplyDelete